Dhumuni la blog hii ni Kudumisha umoja na Kufikisha Taarifa muhimu pamoja na habari mpya kwa wanachama wote wa luwarane popote mlipo.

Search This Blog

Historia ya wachaga



HISTORIA YA WACHAGGA MKOA WA KILIMANJARO

Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 25000. Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kupita yote barani Afrika, umo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Jina la mlima huu ndilo limeupatia mkoa jina lake.

Mkoa wa Kilimanjaro umepakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa kusini na mikoa ya Manyara na Arusha upande wa magharibi. Vikundi vya Wachagga

Wachagga wana historia ndefu ya asili yao na ya maingiliano yao na makabila mengine. Kabila la Kichagga ni mkusanyiko wa makabila madogomadogo (ya Kichagga) yaliyosambaa kijiografia kuzunguka mlima Kilimanjaro kuanzia mashariki (Tarakea, Rombo) hadi magharibi kwa Kilimanjaro (Siha, Machame). wachagga
Kabila la Wachaga linafahamika kwa wengi kuwa linapatikana mkoani Kilimanjaro.Kwa asili, Wachaga ni mchanganyiko wa Wamasai, Wasambaa, Wataita, Wakamba na Wakahe.



Wachaga walianza kuhamia kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro kwenye karne ya 17.



Walipofika wakiwa katika vikundi vidogovidogo waliwakuta wakazi, wenyeji kwenye Misitu ya Mlima Kilimanjaro walioitwa ìWakonyingo..



Wenyeji hawa ambao huitwa Mbilikimo hawakupenda kuchanganyika na wahamiaji wageni, hivyo wakahama na kuanzisha makao yao ya kudumu kwenye misitu minene iliyopo nchini Kongo.



Watu wengi wanafikiria kwamba Wachaga wanatokana na asili moja. Ukweli ni kwamba wamegawanyika katika himaya 15, wanatofautiana kwa lafudhi, lugha, rangi na mwonekano wa miili yao.Wachaga wapo katika makundi makuu matatu ya Hai, Vunjo na Rombo.


Wale wanaopatikana eneo la Hai ni Wasiha, Wamasama, Wamachame,Wangíuni, Wakibosho, Wauru na Wamoshi. Kwa wale wanaopatikana eneo la Vunjo ni Wakirua, Wakilema, Wamarangu, Wamamba na Wamwika.

Kutoka eneo la Rombo ni Wamkuu, Wamashati na Wasseri.
Hadi sasa haijulikani vizuri asili ya jina Wachaga, ila wanahistoria wanaeleza kwamba jina hilo linatokana na neno la Kiswahili linaloitwa 'Kichaka'.

Inaelezwa kwamba misafara ya wafanyabiashara iliyokuwa ikiongozwa na Waswahili pamoja na Waarabu, walipokuwa wakipita maeneo ya Vunjo waliwaona wenyeji wa huko wakiwa wamejenga vibanda vya kulinda mazao yao yasiliwe na wanyama waharibifu.

Wakawaita wenyeji hawa kwamba wanaishi vichakani na kuanzia hapo wageni wafanyabiashara na Wamisionari walipokuwa wanakuja Kilimanjaro walielekezwa na waongozaji misafara yao kwamba wanakwenda kwenye nchi ya ìUchakani,î, wakimaanisha kwamba kwa watu wanaoishi vichakani.

Hatimaye wageni wakashindwa kulitamka vizuri neno hili na kuliita ìUchagani,

Jina hili likawekwa kwenye ramani na kuitwa nchi ya ìWachaga.î Hivyo ndivyo wenyeji waliokuwa wakiishi kwenye Miteremko ya Mlima Kilimanjaro walivyopewa jina lao. Wachaga.



Makabila ya Kichagga ni Wa-Rombo, Wa-Vunjo ambao wanajumuisha watu wa Mwika, Mamba, Marangu, Kilema na Kirua ambayo ndio inajulikana na wengi kama Kirua Vunjo. Ukipenda unaweza kuwagawa watu hawa wa Vunjo kama Wa-Mwika, Wa-Mamba ,Wa-Marangu,Wa-Kilema,na Wakirua.Makabila mengine ni Wa-Old Moshi, Wa-Kibosho, na Wa-Machame, Wa-Uru, na Wa-Siha.
Lugha ya Kichagga
Lugha ya Kichagga inabadilika kuanzia unapotoka Tarakea mpaka unapofika Siha magharibi mlima Kilimanjaro.
Kutokana na tofauti hizo Kichagga kimegawanyika katika Kirombo (ambacho nacho kinatofautiana kadiri unavyotoka eneo moja hadi jingine; mfano Kisseri, Kimashati, Kimkuu, Kimengwe, Kimahida), Kivunjo, Kimarangu, Kirombo, Kioldimoshi, Kingassa, Kiuru, Kikibosho, Kimachame na Kisiha.
Lugha hizo zinakaribia kufanana kadiri makabila hayo yalivyopakana. Kwa mfano, Kivunjo kinafanana na Kioldimoshi. Vile vile Kisiha kinafanana sana na Kimachame ambacho pia kinafanana kidogo na Kikibosho.
Baadhi ya Wamachame walihamia sehemu za Meru, Arusha, na kuchanganyikana na Waarusha, hivyo lugha yao ikabadilika kidogo na kuwa Kimeru. Kwa sababu hiyo Wameru wanasikilizana sana na Wamachame ingawa lafudhi zao zinatofautiana kidogo.
Koo za Kichagga
Majina ya kiukoo ya Kichagga pia huashiria wanatoka sehemu gani ya Uchagga, japo si lazima kuwa hivyo: kwa mfano, familia maarufu za Kichagga nchini Tanzania ni kama ukoo wa akina Mushi, Mmasy Kimaro, Swai, Massawe, Lema, Urassa, Nkya, Ndosi, Meena hutoka Machame.
Akina Temu, Mlaki, Mlay, Lyimo, Moshiro, Mselle, Kamnde, Kileo, Kimambo, Tesha, Msaki, Assey, Kyara, Kessy, Ndanu, Macha, Mbishi, Kombe, Njau wanatoka Old Moshi na Vunjo.
Majina mengine ya Old Moshi ni kama yafuatayo: Mmari, Macha, Mshiu, Kyara, Moshi, Massamu, Kimambo, Mboro, Mlngu, Saule,Tenga, Njau, Malisa, Maro, Maeda, Ringo,Olomi, Ngowi, Lyatuu na mengine mengi.
Kavishe, Mariki, Tarimo, Laswai, Mallya, Mrema, Mkenda, Massawe, Silayo, Lyaruu, Makyao, Mowo, Lamtey, Tairo, Masue, Maleto, Mramba, Kauki wanatoka Rombo.
Sawe, Usiri, Shayo, Kiwelu, Makundi, Urasa, Mtui, Moshi, Meela, Minja, Njau,Mtei wanatoka Marangu na Kilema.
Rite, Makule, Minja, Mashayo, Chao, Shao, Makawia, Ndesano, Kimario, Tilla, Mariale, Tarimo, Mafole, Kituo, Mrosso, Lyakundia, Kessy, Mmbando, Matemba, Ndenshau, Morio, Akaro, Matowo, Towo, Mkony, Temba, Foya, Munishi, Kilawe, na kadhalika hutoka Kibosho.
Utawala wa jadi wa Wachagga
Watawala wa Kichagga waliitwa "Mangi". Hawa walihodhi mashamba, ng'ombe na waliheshimiwa kama viongozi wa kikabila. Walikuwa na nguvu za kisiasa na utajiri. Baadhi ya Ma-mangi mashuhuri katika historia ni kama Mangi Rindi aliyeingia mikataba na wakoloni (Wajerumani), Mangi Sina wa Kibosho na Mangi Horombo wa Keni - waliojulikana kwa uhodari wao wa vita katika kupigana na Wamachame na kupora ng'ombe na mazao yao, hata mpaka leo makabila ya Kimachame na Kikibosho hayaoani kwa urahisi, na Mangi Marealle wa Marangu na Vunjo. Mangi Meli huyu alikuwa mangi wa waoldmoshi ambaye alipigana na wajerumani na aliishia kukatwa kichwa na mpaka sasa kichwa chake kipo ujerumani alizikwa kiwiliwili tuu baada ya kumnyoga na mti aliyonyongewa upo mpaka sasa sehemu ya Oldmoshi bomani karibu na Kolila Sekondari .
Wakoloni walipokuja Kilimanjaro waliingia mikataba na viongozi hawa wa kikabila ili kuweza kuweka misingi yao ya kikoloni. Pia ndugu na watoto wa Ma-mangi walikuwa wa kwanza kupata elimu ya kikoloni, kwa hiyo waliweza kushirikishwa katika serikali za kwanza. Hawa pia wanaaminika walikuwa kama mabepari wa kwanza wa kijadi, maana walifanyiwa kazi na watu wengine wakati wao Ma-mangi wamekaa kuhesabu mali zao.
Usemi maarufu wa "u-Mangi-meza" nadharia inawezekana kuwa umetokana na watawala hawa wa Kichagga.
Elimu kati ya Wachagga
Wachagga wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa katika uwanja wa elimu, hususani katika masomo ya sayansi na hisabati. Moshi ni maeneo ya mwanzo ambayo wamisionari wa Ukristo walijenga makanisa na shule.
Sababu hii imefanya Wachagga kuwa kabila namba moja lenye watu wengi zaidi walio na elimu ya kisasa (elimu ya juu) na mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa idadi ya shule za sekondari nchini Tanzania. Kulingana na takwimu za elimu mkoa huo una shule za sekondari zaidi ya 320. Pia mkoa una shule za msingi zipatazo 950. Idadi hii ya shule ni kubwa zaidi ya idadi ya shule katika mikoa mingine Tanzania.
Shule nyingi za sekondari ziko katika mkoa huu kwa sababu zifuatazo:
 1) Hali ya hewa na vivutio vya kitalii katika mkoa huu viliwavutia zaidi walowezi na wakoloni na kuweka makazi yao hapo. Hivyo wamisionari walijenga shule za kwanza wakifuatiliwa na serikali za wakoloni
2) Serikali ya Tanzania ilirithi shule zilizojengwa na wakoloni
 3) Wachagga waliobahatika kupata fedha binafsi baadaye waliwekeza kwenye ujenzi wa shule binafsi kama kitega-uchumi, wakati wakazi wa mikoa mingine kadhaa walisubiri serikali iwajengee shule.
4) Ukichanganya sababu 1, 2 & 3 utagundua shule katika mkoa Kilimanjaro zimezidi sana idadi ya shule katika mikoa mingine yote.
Ni vema pia kusema kuwa shule hizo huvutia wanafunzi kutoka Tanzania nzima, haziwasomeshi Wachagga tu.
Ardhi
Ingawa ardhi ni msingi wa maendeleo kwa watu wote, kwa Wachagga, ardhi ni mali sana kwa sababu kilimo chao ni cha mazao ya kudumu kama kahawa na ndizi hukaa shambani kwa muda wa miaka mingi.
Mojawapo ya urithi wapewayo watoto ni "kihamba". Hii ni sehemu ya ardhi ambayo mtoto anategemewa atajenga na kuanzisha familia yake. Bahati mbaya watoto wa kike walikuwa hawapewi kipaumbele katika ugawanaji wa vihamba. Uhaba wa ardhi huko Uchaga ulipelekea Wachagga wengi kuhamia mikoa mingine. Hivi leo utakuta Wachagga wakiishi Dodoma, Morogoro, Iringa, Mbeya n.k. wakiwa wamepanda migomba yao na kuendesha biashara za maduka ya vyakula.
Ukienda kwenye mikoa hiyo utakuta wamejenga jamii zao na vyama vyao vya kusaidiana wakati wa sherehe au matatizo. Aidha hata pombe ya mbege utaweza kuikuta kwenye makusanyiko ya Wachagga katika mikoa mbalimbali.
Kilimo na chakula
Wachagga hulima mazao ya chakula kama vile mahindi, maharagwe, viazi, ndizi, ulezi na mboga mbalimbali.Kuna vyakula na mazao ya kienyeji kama vile viazi vikuu, majimbi “sowe” “shiha”pia matunda ya maparachichi,matimamti,flaumene Matunda posi Msambochi, ndaraho,ndawiro nk.  Pia mazao ya biashara kama vile kahawa, nyanya na vitunguu.

Ndizi za Wachagga
Ingawa Wachagga wa leo wanakula vyakula mbalimbali kama vile ugali, wali na viazi, chakula kikuu cha Wachagga ni ndizi.
Kuna ndizi za aina mbalimbali na kwa matumizi tofauti. Mfano ndizi sukari ni fupi na huachwa hadi ziive na huliwa mbivu kama tunda.
Ndizi mshare,Mrhirhiwe,Mkonosi, Ndishi,Matoke, Kitarasa hukatwa zikiwa mbichi na kupikiwa vyakula mbalimbali pamoja na nyama ya ng'ombe, kondoo au mbuzi. Mara nyingine hupikwa na maharage, choroko, kunde,mrhondo,  au hata maziwa ya mtindi. Vyakula vya ndizi huja kwa ladha tofauti kama vile ndizi nyama, mtori, machalari, kiburu na kadhalika.
Aina nyingine ni ndizi ng'ombe (mrharhao,kipungarha )ambazo huachwa ziive halafu humenywa na kutumiwa kutengenezea pombe maarufu iitwayo mbege. Mbege hutengenezwa kwa kutumia ndizi mbivu, maji, na ulezi.
Aina nyingine ni ndizi mzuzu. Hizi zikikomaa huachwa zianze kuiva kidogo halafu huchomwa na kuliwa kama kitafunwa pamoja na chai au pombe. Ukipita mitaa ya Dar es Salaam utaona ndizi mzuzu zikichomwa sambamba na muhogo au kuku vumbi au kiti moto.

Maendeleo ya Wachaga

Maendeleo yao hapo awali yalitokana na zao la kahawa. Walifanikiwa kuanzisha vyama vya ushirika na hatimaye mwaka 1932 walianzisha Halmashauri ya Wachaga (Chaga Council) ambayo kwa sasa inatumiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

Halmashauri hii iliongozwa na Mangi Mkuu ìMshumbue Thomas Marealle II.



Mwaka 1946, utawala wa Waingereza uliboresha Baraza la Halmashauri ya Wachaga. Himaya ndogo za Wachaga zipatazo 17 (himaya mbili za Wakahe na Waarusha chini zilijumuishwa kwenye Tarafa ya Vunjo) na kuundwa kwa Tarafa tatu za Hai, Vunjo na Rombo.



Halmashauri ya Wachaga ilijenga miundombinu na huduma za jamii ikiwamo kuwasomesha watoto wao kwenye shule na vyuo mbalimbali kama Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda.



Halmashauri ya Uchaga ilikuwa na bendera yake ambayo ipo hadi leo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, yenye nembo tano kuu:


1- Mlima Kilimanjaro uliochorwa katikati ya bendera ukionyesha mandhari nzuri ya kilele cha Kibo. Kilele cha Kibo kinatoa maji safi na ni kielelezo cha umoja wao.

2- Chini ya kilele cha Kibo, upande wa kushoto wa bendera kuna mgomba wenye ndizi. Hiki ni chakula kikuu cha Wachaga.

3- Upande wa kulia wa bendera ni tawi la mbuni ukiwa na matunda yake. Kahawa ni zao lililowaletea maendeleo.

4- Bendera imezungukwa na matawi ya 'sale' lenye matawi mawili (draceana plant). Matawi haya yamefanya mduara kuzunguka kilele cha Kibo, mgomba wa ndizi na tawi la zao la kahawa. Masale ni mmea unaoheshimiwa sana na Wachaga wote.

Ni alama ya amani. Masale hutumika katika sherehe na shughuli zote za kimila zinazofanywa na Wachaga. Majani yake ni kijani kibichi yanayoonyesha jinsi Kilimanjaro ilivyo na rutuba nzuri inayostawisha mazao ya kila aina.

5- Juu kidogo ya kilele cha Kibo yupo chui ambaye amejipumzisha. Chui ni alama kuu ya mamlaka ya Wachaga.

Hapo awali kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro walikuwepo chui wengi wa rangi nyeusi lakini kutokana na ongezeko la watu pamoja na uharibifu wa mazingira chui hawa wametoweka.


Sikukuu ya Wachaga
Sikukuu ya Wachaga wote ilikuwa ikiadhimishwa Novemba 10 kila mwaka kama kumbukumbu ya siku ambayo Wachagga wote walipokusanyika na kumchagua Mangi Mkuu baada ya kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya Uchagga.

Halmashauri hii iliongozwa na Mangi Mkuu ìMshumbue Thomas Marealle II.

Mwaka 1946, utawala wa Waingereza uliboresha Baraza la Halmashauri ya Wachaga. Himaya ndogo za Wachaga zipatazo 17 (himaya mbili za Wakahe na Waarusha chini zilijumuishwa kwenye Tarafa ya Vunjo) na kuundwa kwa Tarafa tatu za Hai, Vunjo na Rombo.

Halmashauri ya Wachaga ilijenga miundombinu na huduma za jamii ikiwamo kuwasomesha watoto wao kwenye shule na vyuo mbalimbali kama Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda.

Halmashauri ya Uchaga ilikuwa na bendera yake ambayo ipo hadi leo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, yenye nembo tano kuu:

1- Mlima Kilimanjaro uliochorwa katikati ya bendera ukionyesha mandhari nzuri ya kilele cha Kibo. Kilele cha Kibo kinatoa maji safi na ni kielelezo cha umoja wao.

2- Chini ya kilele cha Kibo, upande wa kushoto wa bendera kuna mgomba wenye ndizi. Hiki ni chakula kikuu cha Wachaga.

3- Upande wa kulia wa bendera ni tawi la mbuni ukiwa na matunda yake. Kahawa ni zao lililowaletea maendeleo.

4- Bendera imezungukwa na matawi ya 'sale' lenye matawi mawili (draceana plant). Matawi haya yamefanya mduara kuzunguka kilele cha Kibo, mgomba wa ndizi na tawi la zao la kahawa. Masale ni mmea unaoheshimiwa sana na Wachaga wote.

Ni alama ya amani. Masale hutumika katika sherehe na shughuli zote za kimila zinazofanywa na Wachaga. Majani yake ni kijani kibichi yanayoonyesha jinsi Kilimanjaro ilivyo na rutuba nzuri inayostawisha mazao ya kila aina.

5- Juu kidogo ya kilele cha Kibo yupo chui ambaye amejipumzisha. Chui ni alama kuu ya mamlaka ya Wachaga.

Hapo awali kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro walikuwepo chui wengi wa rangi nyeusi lakini kutokana na ongezeko la watu pamoja na uharibifu wa mazingira chui hawa wametoweka.

HISTORIA YA UKOO


Kutokana na histora inavyojitanabahi ukoo wa akina Temu ni ukoo wa asili katika kabila la Wacchaga ikiwa asili yao ni kutoka kwa wakamba
Mila za ukoo bado ni nzuri kuzingatia maadili tuliyopewa na mababu zetu.
Hapo awali wazee wa ukoo walikuwa ni wanuwezo mkubwa katika uongozi na waliweza kuchaguliwa kama mchili na kwenye mabaraza ya mangi, pia walikuwa na maone katika elimu ni miongoni mwa ukoo wenye wasomi pia ni matajiri wa awali. walikuwa na mali kama za mashamba nyuma kwa maana kulikuwa na wahunzi (wengine wakapatiwa mchuma) hodari wa ufundi hasa kutengeneza silaha za kijadi mkuki (iphumu, soka, mndo, chumbuo nk) Wazee wakotemu walikuwa wafugaji na wafanya biashara za kubadilishana.
Ukoo wetu hutaweza kuona makaburi ya zamani sana kwani ilikuwa hawaziki bali ilikuwa wanahifandhi katika nyumba ya nyasi ambayo ilikuwandio nyumba ya asili ndiko mwili ulihifadhiwa na kufunikwa na mbolea kwa muda wa miaka mitatu na baadae mifupa ilichukuliwa na kuwekwa mahali maalum ambapo palijulikana kama (mbuwonyi) ni eneo la kuchinjia na kutole mitambiko mbalimbali kulingana na hitaji. Umoja wa ukoo ulikuwa ni makini wakotemu walikuwa hawasahauliani wakichinja ni lazima kumuita ndugu au kumpelekea nyama kuonyesha ishara ya upendo. Pia walialikana kalam kuna msiba au sherehe utakuta kila mtu anachangia ndizi,mbuzi na nguvu kazi kufanikisha shughuli hiyo. Ukoo wa Akina Temu ndio ulikuwa na wasomi wa mwanzo wa Kichagga.
Pia katika ujezi yule ndugu ambaye alionekana mnyonge walialikana na kumchangi ujenzi wa nyumba enzi hizo ni nyasi hivyo walijipanga wakukata fito,nyasi,wakubeba mawe kwa ajili ya msingi na (moondi wo umbe na koombe)Ukoo wa temu hauna magonjwa ya kurithi ni watu na afya zao. Katika ukoo kila mzee wa familia alimtafutia motto wake sehemu ya kuishi (kiwamba) na ikiwa hakua eneo aliweza kutafuta pengine kwa kununua.
Nyumba hizo za asili kwa sasa zimekuwa adimu na mahali pa kuweza kuziona ni makumbusho ya vitu vya asili na utamaduni wake.

Nyumba hii iikuwa na sehemu mbalimbali zilizokuwa zinajulikana kama ifuatavyo:- 
Kuna koombe –sehemu ya mifugo Kimolya – sehemu ya mbele ya kuhifadhia vitu muhimu sana na hakuruhusiwa watoto kufika huko 
Kuna Kiwangowangonyi- kuhifadhia panga au mundu 
Kuna mrwawenyi – kuhifadhia chimbio Kuna moou – sehemu ya malisho ya mifugo 
Kuna kai – ni dari sehemu ya kuvundikia ndizi Upurhunyi – sehemu ya nyuma ya mifugo ya kutolea mikojo ya ng’ombe na mbuzi 
Kuna eneo la kichinyi au ulyii eneo la kulala Pia nyuma ya nyumba kwa nje ilijulikana kama Karhii ambapo kma kuna dharura,maongezi ya siri yalifanyikia eneo hili na liliheshimika huwezi kubisha hodi na kwenda moja kwa moja enoe hilo,pia ni sehemu ya kuogea


Ukoo wa akina Temu kam historia inayozungumza imegawanyika katika makundi matatu mpaka manne
  • Kuna Temu toka Kilema juu karibu na maua mpaka Ngangu na maeneo chini yake kidogo
  • Kuna Temu iliyopo sembeti na ikavuka mpaka kilema chini maeneo ya masaera
  • Kuna Temu iliyopo Mamba, mwika, mpaka Mamsera
NB. UkooTemu iliyopo Babati,Sanya Juu wote ni wahamiaji lakini asili yao ni kutoka maeneo tajwa hapo juu.Pia kuna Temu wapo Kenya mmoja  alikuwa Anaitwa Naftali Temu alishinda mbio huko Mexico pia kuna mtangazaji  TV nae Temu hivyo utaona historia inavyozunguka ni baadhi ya babu zetu katika harakati za kutafuta maisha hadi Kenya.
Ikumbukwe kuwa zamani watoto waliokuwa wana zaliwa walikuwa wachache pia walikuwa wanashambuliwa na magonjwa hivyo kujikuta ukoo unakuwa hauongezeki hivyo babau zeu walisafiri kwenda eneo lingine kuowa na kuongeza familia ndipo Ukoo ukajikuta umetawanyika ingawa chanjo ni kimoja pia inasadikika kuna wengine walitofautiana mtu na mdogo wake anahamia sehemu nyingine na kuwanya ukoo kukua na kusambaa.
Imani (dini)
Ukoo wa akina Temu ni ukoo kongwe hivyo kama inavyojulika walikuwa wasomi wengi wa mababu zetu walishirikiana na wamissionari waliofika katika maeneo yetu hivyo walijikuta wakiwa katika dini mbili za awali Lutheran na Roman catholic
Kundi la Ukoo walipitia kilema wengi wao Roman Catholic walioelekea Mamba na Mwika wengi wao wanasali Lutheran lakini Temu ya Marangu Sembeti, Kilema chini ni mchanganyiko wa Roman Catholic,Islamic na Lutheran ingawa imani hizo hazikutengua undugu wa ukoo.
Kuna mila za ukoo ambazo bado zinafuatutiliwa ili ziwekwe kwenye machapisho ambazo utafiti wake umekamilika mfano:
Kupokea mtoto aliyezaliwa ndani ya ukoo
Kuombana msamaha ndugu wakikoseana
Baba na mama wakipigana taratibu za kurusiana
Kuzaa na mke wa mtu ni kuvunja heshima ila kuna taratibu
Kuzaa na ndugu kwa bahati mbaya bila kujuana
Kumtuhumu ndugu kwa kumlaani ndugu yako /viapo/leka
Taratibu za kuoa ukoo mwingine
Mazishi ya mtu mzima baba/mama/babu na nk
Mwana ukoo aliyefia mbali na kuzikwa huko taratibu za kumrudisha nyumbani
Kushikwa ugoni na mke wa mtu taratibu zake
Utaratibu wa kuarifu ukoo kuhusu harusi ya mtoto me/ke




By Fulgence Edward Chezamkono Tisira Temu.

No comments:

Post a Comment